Home Kitaifa WEKENI BEI NAFUU YA GESI KWA WANANCHI – DKT. MWINYI

WEKENI BEI NAFUU YA GESI KWA WANANCHI – DKT. MWINYI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduz, Dk. Hussein Ali Mwinyi akikata utepe kuzindua bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group of Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024 Mangapwani Zanzibar. Wengine kutoka kulia ni Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Injinia Zena Ahmed Said, Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Ltd, Benoite Araman, Mwenyekiti wa makampuni ya Vigor, Taufiq Salum Turky na kutoka kushoto ni Katibu wa NEC itikadi, uenezi na mafunzo CCM Zanzibar, Khamis Mbeto, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Hadid Rashid Hadid na Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Shaib Hassan Kaduara.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akikata utepe kuweka jiwe la msingi kuzindua bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx uliofanyika leo Juni 27, 2024 huko Mangapwani Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akipanda mti baada ya kuzindua bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx uliofanyika leo Juni 27, 2024 huko Mangapwani Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Mhandisi wa Kampuni ya Oryx, Joseph Soka alipokuwa akitoa maelezo wakati wa hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati za gesi ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024 Mangapwani Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameyaomba makampuni ya gesi kutafuta namna ya kuwezesha kupatikana gesi kwa bei nafuu, ili wananchi wamudu bei ya bidhaa hiyo kwa matumizi ya kupikia.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 27 Juni 2024 alipofungua rasmi Bohari ya kwanza ya kuhifadhia Gesi ya Kampuni ya Oryx Gas Zanzibar Limited iliyopo Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ametoa rai kwa wananchi kuondokana na matumizi ya makaa na kuni hatua kwa hatua kwa ajili ya nishati ya kupikia, ili kupunguza athari za mazingira pamoja na kujiepusha na athari za kiafya zinazotokana na hewa sumu.

Rais Dkt. Mwinyi amepongeza uwekezaji wa Kampuni ya ORYX Gas Zanzibar Limited kwa kujenga matangi mawili yenye ujazo wa tani 1,388 sawa na kilo 1,388,000 za gesi.

Kwa upande mwingine, Rais Dkt. Mwinyi amesema kila mwananchi aliyehamishwa eneo la bandari jumuishi ya Mangapwani atalipwa fidia stahiki na makazi mbadala bila wasiwasi wowote.


LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!