Home Kitaifa WAZIRI NDALICHAKO ATETA NA MENEJIMENTI YA OFISI YAKE

WAZIRI NDALICHAKO ATETA NA MENEJIMENTI YA OFISI YAKE

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekutana na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Ofisi hiyo leo tarehe 7 Juni, 2023 katika jengo la OSHA, jijini Dodoma.

Lengo la kikao hicho ni kufanya majadiliano kuhusu maendeleo ya ukarabati wa Vyuo vinne (4) vya Ufundi Stadi na Marekebisho kwa Watu wenye Ulemavu, hatua iliyofikiwa ujenzi wa Vyuo vitatu (3) vya Watu wenye Ulemavu, Mpango wa Taifa wa Watu wenye Ualbino na Madeni ya Waajiri ambao hawajawasilisha michango kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Prof. Ndalichako pia amewataka viongozi hao kuendelea kuchapa kazi kwa weledi na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao ili kufikia azma ya Serikali na wananchi wanaowahudumia. Vile vile, Mhe. Ndalichako amesisitiza menejimenti hiyo kuendelea kutangaza mafanikio na mambo makubwa yanayofanywa na serikali kwa maslahi ya taifa.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!