Home Biashara WATANZANIA 28,600 WAVUNA MAMILIONI YA TIGO CHA WOTE

WATANZANIA 28,600 WAVUNA MAMILIONI YA TIGO CHA WOTE

Washindi  elfu ishirini na  nane mia sita (28,600) wamepatikana kwenye kampeni ya Cha wote kutoka tigo tokea kuanza kwa kampeni hiyo iliyodumu kwa siku tisini 

Hayo ameyasema Mary Rutta  Meneja wa kitengo Maalum tigo pesa leo Septemba 22, 2023 wakati akikabidhi baadhi ya wawakilishi zawadi ya hundi ya milioni Moja Ofisi za Tigo Jijiji Dar es salaam   

Ameongezea kwa kusema watumiaji wa mtandao huo waendelee kuwa karibu na huduma zao kwani kuna mambo kibao yatakayokuja kwa wateja wao 

Naye Mshindi Devotha Kweka  kutokea Dar es salaam amejishindia milioni moja amesema fedha hizo zitamsaidia kukuza biashara yake na mambo yake binafsi

Kampeni hiyo ikiwa imefikia tamati  imedumu kwa siku tisini miongoni mwa zawadi zilizokuwa zinatokewa ni Milioni tano bonasi ya dakika na SMS

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!