Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuwa kwa sasa hali ya chakula ni nzuri na ya kutosha hivyo Serikali itachukua hatua kuhakikisha inawapa unafuu wananchi kuelekea Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, aidha Rais Dk. Mwinyi ameongezea na kusema wafanyabiashara ambao watahodhi vyakula watashitakiwa kwa kosa la Uhujumu wa Uchumi.
Rais Dk.Mwinyi aliyasema hayo leo katika Mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Ikulu Zanzibar leo tarehe 28 Februari , 2023.