Home Michezo TARIME VETERAN MABINGWA BONANZA LA MAKARIBISHO YA RC MTANDA

TARIME VETERAN MABINGWA BONANZA LA MAKARIBISHO YA RC MTANDA

Na Shomari Binda-Musoma

TIMU ya Tarime veteran wameibuka mabingwa wa bonanza maalum la nane nane kumkaribisha mkuu wa Mkoa wa Mara Said Mtanda.

Kwa kutwaa ubingwa huo timu hiyo imeondoka na zawadi ya ng’ombe pamoja na kombe na kuzishinda timu nyingine 5 zilizoshiriki bonanza hilo.

Katika mchezo wa fainali Tarime veteran imeifunga timu ya 27 KJ Makoko kwa changamoto ya mikwaju ya penati 4-2

Timu nyingine zilizoshiriki bonanza hilo ni Musoma veteran, Mara veteran, Biashara United veteran na Butiama veteran.

Akihitimisha bonanza hilo baada ya kutoa zawadi kwa washindi,mkuu wa mkoa wa Mara Said Mtanda amewashukuru waandaji wa bonanza hilo timu ya Biashara United veteran na kusema wameandaa jambo kubwa.

Amesema yeye ni mwanamichezo na yupo tayari kushiriki kwenye jambo lolote la kimichezo na kuomba ushirikiano kwa viongozi wa michezo.

RC Mtanda amesema mkoa wa Mara una wanamichezo wengi na kuahidi kushirikuans na kila mmoja ikuwemo kuisaidia timu ya Biashara United inayoshiriki ligi daraja la kwanza na hatimaye kurejea ligi kuu.

Mwenyekiti wa Biashara United veteran, Dommy Mkono.amesema wataendelea kuandaa michezo mbalimbali kwa kushirikiana na ofisi ya mkuu wa mkoa.

Dommy amesema wanamshukuru mkuu wa mkoa kwa kutoa zawadi ya ng’ombe kwa mshindi pamoja na wadhamini wengine.

Kwa upande wa timu zilizoshiriki bonanza hilo wamewashukuru waandaji kwa kuandaa bonanza hilo ns kuwapa burudani.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!