Home Biashara TANZANIA NA MAREKANI KUIMARISHA UHUSIANO WA KIBIASHARA NA UWEKEZAJI

TANZANIA NA MAREKANI KUIMARISHA UHUSIANO WA KIBIASHARA NA UWEKEZAJI

Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano wa kibiashara na uwekezaji baina yake na Marekani na inawakaribisha wawekezaji kutoka nchini humo kuja kuwekeza na kushirikiana na watanzania katika ufanyaji biashara katika sekta mbalimbali nchini.

Dkt. Kijaji ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo kuhusu kuendeleza uhusiano wa kibiashara na uwekezaji baina ya nchi hizo na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Michael Battle Machi 27, 2023 katika Ofisi ndogo ya Wizara, jijini Dar es Salaam.

Aidha, Waziri Kijaji ameiomba Marekani kuongeza muda wa Mkataba wa Mpango wa Ukuzaji fursa za Kiuchumi Afrika (AGOA) uliotiwa saini mwaka 2000 na awamu inayotarajiwa kuisha ni kati ya 2015 na 2025.

Akifafanua zaidi, Dkt. Kijaji amesema Mpango huo wa AGOA unalenga kutoa fursa ya upendeleo kwa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara kupeleka bidhaa zaidi ya 6,500 bila kulipa ushuru wa forodha nchini Marekani

Dkt. Kijaji pia ameainisha kuwa Tanzania ni moja ya nchi inayonufaika na fursa ya Mpango wa AGOA ambapo Sekta ya Nguo na Mavazi inachangia mauzo kwa asilimia 95. Kutoka katika Viwanda vikubwa vya Mazava Fabrics and Production E.A L, na Tanzania Tooku Garments Co., Ltd . Bidhaa zingine zinazochangia asilimia 5 ni bidhaa za Mikono, Uchakataji bidhaa za kilimo (Agro-processing) na Ngozi.

Naye Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Michael Battle amesema Marekani itaimarisha uhusiano wa kibiashara na uwekezaji na Tanzania hususani katika sekta mbalimbali ikiwemo viwanda na kufanya biashara na benki za kitanzania ili kirahisisha upatikanaji wa mitaji kwa wafanyabiashara wa Tanzania.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!