Home Kitaifa SERIKALI KUHAKIKISHA MISAMAHA YA KODI INATUMIKA IPASAVYO

SERIKALI KUHAKIKISHA MISAMAHA YA KODI INATUMIKA IPASAVYO

Na Farida Ramadhani, WFM – Dodoma

Serikali imesema inaendelea kutekeleza sheria katika ufuatiliaji na tathmini ya misamaha ya kodi ikiwemo Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ili kuhakikisha kuwa misamaha ya kodi inatolewa kwa kuzingatia sheria na inatumika kama ilivyokusudiwa.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kibamba, Mhe. Issa Jumanne Mtemvu aliyetaka kujua mkakati wa Serikali kuhakikisha Misamaha ya VAT inayotolewa inaleta tija kama ilivyokusudiwa.

Mhe. Chande alisema ili kuhakikisha misamaha ya kodi inakuwa na tija katika uchumi na jamii kwa ujumla, orodha ya bidhaa na vifaa vinavyostahili msamaha wa kodi inaandaliwa na kuhakiki orodha ya bidhaa na vifaa.

Tunahakikisha mwombaji anajaza fomu maalum inayothibitisha ununuzi wa bidhaa au vifaa husika pamoja na kufanya kaguzi za mara kwa mara dhidi ya misamaha iliyotolewa ili kuthibitisha iwapo matumizi ya bidhaa au vifaa vilivyosamehewa kodi vimetumika kama ilivyokusudiwa”, aliongeza Mhe. Chande.

Alisema pia Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea kutekeleza matakwa ya kisheria katika ufuatiliaji na tathmini ya misamaha ya kodi ikiwemo Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ili kuhakikisha kuwa misamaha ya kodi inatolewa kwa kuzingatia sheria na inatumika kama ilivyokusudiwa.

Mwisho.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!