Home Michezo MTOKO WA KIBINGWA WAIPAMBA LUPASO, DERBY YA KARIAKOO MNYAMA APETA

MTOKO WA KIBINGWA WAIPAMBA LUPASO, DERBY YA KARIAKOO MNYAMA APETA

WASHINDI wa Promosheni ya Mtoko wa Kibingwa wa Betika wa hitimisa Msimu wa 5 na Bata la Kibabe  na kutazama Derby ya Kariakoo kati ya Simba na Yanga Jana  Aprili 16,2023 ambapo Mnyama aliibuka na Bao 2 Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es salaam. 

Akizungumza mara baada ya Kumalizika kwa Derby hiyo Afisa Uhusiano wa Betika Nelson Pius amesema Kumalizika kwa Mtoko wa Kibingwa Msimu wa 5 tayari umekamilisha idadi ya washindi 400 ambapo kwa msimu ujao washindi wataongezeka ili kuwapa nafasi zaidi kupata Bata la mtoko wa kibingwa huku akikiri kuwa Mabingwa hao wamekata kiu yao ya kutazama Mechi hiyo ya watani wa jadi Simba na Yanga Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es salaam. 

Hata hivyo mabingwa hao walipata huduma za kipekee (special treatment)  Hoteli ya nyota tano pamoja na Kushuhudia Derby hiyo ya Kariakoo wakiwa wamekaa viti vya vip A.

Pius ameongeza kuwa Mabingwa hao 100 kutoka Mikoa mbalimbali wataenda kuwa mabalozi wazuri kwa wengine ambao wataguswa kutupia ubashiri kwenye Kampuni ya betika kwani betika ina Kitonga deile jackpot kwa dau la 250 na huku Mtoko wa kibingwa unakuhitaji dau la shilingi 500 kwa mikeka mitano ushinde au usishinde tayari unapata tiketi ya moja kwa moja kuingia kwenye droo hiyo.

Pia amesema msimu wa 6 wategemee mengi zaidi na kufanya ubashiri wao na yoyote anaeweka ubashiri anaingia kwenye droo ya Mtoko wa Kibingwa hauna Mbambamba ambapo mtoko huo utachukua idadi kubwa zaidi kufikia zaidi ya 150 lengo ni kuwapa nafasi watu wengine kupata bata la kibingwa kutazama Mechi kubwa ikiwezekana hata Ligi kubwa nje ya nchi.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!