Na Mwandishi Wetu
Kampuni namba moja nchini kwa utoaji wa huduma za Kidigitali Tigo Tanzania kupitia Huduma yake ya mfumo wa pesa Kidigitali Tigo Pesa , imetoa zawadi kwa Mawakala wake Wakubwa na Wadogo kutoka Tanzania Bara na Visiwani ikiwa ni sehemu ya kuhitimisha Kampeni yake iliyofanya vizuri ya WAKISHUA .
Akizungumza Usiku wa tukio hili la kihistoria lililofanyika Jijini Dar Es Salaam Afisa Mkuu wa Tigo Pesa Bi. Angelica Pesha amesema
” Tukio la leo ni kwa ajili ya Mawakala wetu wakubwa na wadogo wanaotusaidia Kila siku ili kuweza kuwafikia wateja wetu na kuwapa huduma za Tigo Pesa , tumeona tujumuike nao kusheherekea mafanikio yetu ya mwaka 2022 sambamba na hayo tutatoa Zawadi Mbalimbali kwa mawakala wetu waliofanya vizuri , akiwemo Bi. Neema Swai atajipatia Milioni 15 akiwa kama wakala aliyefanya miamala mingi zaidi kwa Mwaka 2022 “
Wengine ni Said Khatibu Wakala kutoka Zanzibar ambaye ndiye mmoja wa wakala aliyetoa huduma kwa mda mrefu zaidi na kwa mawanda mapana .
Wakala Waziri Omary kutoka Kibaha ambaye ni wakala aliyefanya Vizuri katika kanda ya Pwani , na Saba General Enterprises Limited ambaye huyu ni Wakala ambaye anafanya miamala kiufasaha yaani hana malalamiko ya wateja ” . Alimalizia
Kwa upande wake Bi . Neema Swai Mshindi wa Milioni 15 kutoka TIGO PESA kama wakala aliyefanya miamala mingi zaidi , ameipongeza Kampuni ya Tigo kwa kuamua kuwakumbuka Mawakala wake kwa kuwazawadia zawadi mbalimbali na kuwakutanisha pamoja .