Home Kitaifa MCHINJITA AKOSOA SERA ZA KILIMO ZA WAZIRI BASHE

MCHINJITA AKOSOA SERA ZA KILIMO ZA WAZIRI BASHE

Aliyekuwa mgombea wa jimbo la Namtumbo, Bonifasia Mapunda, akifurahia jambo na vijana wa jimbo hilo.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Bara, Issiaka Mchinjita, wa pili kutoka kulia, akizungumza na wafanyabiashara wa Gulio Njalamatata katika kata ya Mkongo, jimbo la Namtumbo, mkoani Ruvuma.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Bara, Issiaka Mchinjita, akimsajili mwanachama mpya kwa njia ya kidigitali katika kata ya Mkongo, jimbo la Namtumbo, mkoani Ruvuma.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Bara, Issiaka Mchinjita, akigawa kadi za kielektroniki kwa wanachama wa chama hicho katika kata ya Mkongo, jimbo la Namtumbo, mkoani Ruvuma.

Na Ritha Jacob – Ruvuma

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Bara, Issiaka Mchinjita, ametoa wito kwa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, kumtafutia wakala wa mbegu eneo maalum la kulima mbegu zake ili kuwaachia wananchi mashamba yao. Hatua hiyo itawezesha wakulima kuzalisha mazao yanayotumika kulisha Watanzania.

Mchinjita alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi wa Jimbo la Namtumbo mkoani Ruvuma, alipokuwa akiendelea na ziara yake ya kutembelea mikoa sita, iliyoanza Julai 22, 2024. Ziara hiyo ina lengo la kusajili wanachama milioni 10 kwa miezi 10 na kusikiliza wananchi.

Waziri Bashe ameanzisha mashamba ya BBT kule Dodoma, ni vyema akaelekeza wakulima wa mbegu huko badala ya kuwafukuza wananchi na wakulima kutoka mashamba yao. Kama serikali ina ardhi ya kutosha kiasi cha kuwahimiza vijana wote waliokosa ajira kuenda kulima, kwa nini wakulima wanatolewa kwenye mashamba yao?” alisema Mchinjita.

Aidha, aliongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma unaongoza kwa uzalishaji wa makaa ya mawe, ambayo yanapelekwa kwenye mikoa mingine yenye viwanda. Mkoa huo hauna viwanda ambavyo vingesaidia kuzalisha malighafi zinazopatikana hapo, hatua ambayo ingewasaidia wananchi kupata vipato na vijana kupata ajira.

Mchinjita pia alizungumzia kuhusu mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 600 kwa kutumia makaa ya mawe, ambao haujaendelea. Alisema mradi huo ungeweza kuchochea uwekezaji kwa kuhakikisha upatikanaji wa nishati na hivyo kuvutia wawekezaji kutoka duniani kote kuwekeza katika malighafi zinazopatikana Ruvuma.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!