Home Biashara MAFUNDI MOROGORO WAIPOKEA KIBOKO WALL PUTTY KWA KISHINDO , WASHUHUDIA MABORESHO YA...

MAFUNDI MOROGORO WAIPOKEA KIBOKO WALL PUTTY KWA KISHINDO , WASHUHUDIA MABORESHO YA RANGI ZA KIBOKO

 .

Baadhi ya Mafundi kutoka Morogoro Mjini na maeneo ya Karibu katika semina iliyoandaliwa na kampuni ya Utengenezaji , Uuzaji na Usambazaji wa Vifaa vya Ujenzi nchini ya KIBOKO PAINTS ambapo kampuni hiyo imetambulisha bidhaa yake mpya ya KIBOKO WALL PUTTY kwa mafundi hawa , sambamba na hilo KIBOKO PAINTS imemtambulisha Muigizaji Salim Ahmed ( Gabo Zigamba  )  kama Balozi wake, utambulisho uliofanywa na Afisa Masoko Mkuu wa Kampuni ya KIBOKO PAINTS Bwn. Erhard Mlyansi ( pichani , picha ya 1 ) Leo Julai , 12 , 2024 katika Ukumbi wa Mount Uluguru Hotel Morogoro Mjini.

Muigizaji Gabo Zigamba balozi wa Kampuni ya KIBOKO PAINTS ( katikati ) , Afisa Masoko Mkuu wa Kampuni ya KIBOKO PAINTS Bwn. Erhard Mlyansi ( kushoto ) na Pankaj Tiwari – Meneja Mauzo KIBOKO PAINTS Tanzania katika semina ya Utambulisho wa KIBOKO WALL PUTTY kwa mafundi mapema leo hii , Morogoro Mjini.




 Mafundi wakiifanyia majaribio kwa kuipaka ubaoni bidhaa ya KIBOKO WALL PUTTY  mbele ya wenzao ili kujionea ubora wake , Aidha Mafundi hawa wamezijaribu rangi za KIBOKO na kuyashuhudia maboresho makubwa ambayo kampuni imeyafanya katika rangi  hizo.

Na Adery Masta. 

Kampuni namba moja nchini kwa uuzaji wa Vifaa mbalimbali vya Ujenzi kama vile Mabati , Rangi n.k  KIBOKO Paints, Imetambulisha Bidhaa yake mpya sokoni ya KIBOKO WALL PUTTY yenye Ubora wa hali ya juu kwa baadhi ya Mafundi Rangi wanaoishi na kufanya kazi maeneo ya Morogoro Mjini.

 Leo , Julai, 12 , 2024 akizungumza baada ya Semina , Bwn. Hamidu Satara ambaye ni Afisa Mauzo wa kampuni, lakini pia Mkufunzi wa Semina hiyo amesema 

” Kampuni ya KIBOKO PAINTS inafanya Semina hizi nchi nzima ambapo kwa upande wa Dar Es Salaam tumefanya Gongo la Mboto na maeneo yake ya karibu , Buguruni na maeneo yake ya karibu , Mbezi , Kariakoo , Mbagala na  Kigamboni na kwa hapa Morogoro zitafanyika Morogoro Mjini na Ifakara , kisha Dodoma itafuata , Hakika niwapongeze mafundi wa Morogoro Mjini kwa muitikio wao mkubwa katika kuhudhuria semina hii na tumeelezana mengi kuhusu Bidhaa yetu mpya ya WALL PUTTY lakini pia na maboresho makubwa tuliyoyafanya katika rangi zetu ” amesema Bw. Hamidu

Stephano ni fundi rangi aliyezungumza na Mwandishi Wetu Baada ya Semina hiyo ameipongeza kampuni ya KIBOKO PAINTS kwa kuileta sokoni KIBOKO WALL PUTTY yenye Ubora wa hali ya juu 

“KIBOKO WALL PUTTY ni Bora sana ukiitumia hutopata gharama ya kununua material mengine tofauti ya kufanya Skimming , KIBOKO PAINTS wamefanya maboresho makubwa na kuja na Wall putty Bora kuliko nyingine zilizopo sokoni “ amesema.

Aidha Bwn . Stephano ameipongeza kampuni ya KIBOKO kwa kufanya maboresho makubwa katika rangi zake, kwa sasa ni miongoni mwa rangi bora zaidi sokoni.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!