Home Michezo MABINGWA WATETEZI NYASHO FC WAICHAPA KIGERA FC 6-0 MATHAYO CUP

MABINGWA WATETEZI NYASHO FC WAICHAPA KIGERA FC 6-0 MATHAYO CUP

Na Shomari Binda-Musoma

MABINGWA watetezi wa mashindano ya Mathayo Cup msimu uliopita, Nyasho fc wameanza vyema kutetea ubingwa wao baada ya kuifunga timu ya Kigera bao 6-0

Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Nyasho walikuwa mbele kwa uongozi wa mabao 2-0 huku wakionekana kutawala mchezo huo.

Kipindi cha pili Nasho walionekana kuendelea kuutawala mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa Mara sekondari na kuongeza mabao mengine 3.

Kufuatia kichapo hicho kocha wa timu ya Kigera,Kapuru Kapuru,amesema wachezaji wake wameshindws kufuata maelekezo yake na kupelekea kupoteza mchezo huo.

Amesema anakwenda kufanyia kazi makosa yaliyoonekana ili kuweza kupata ushindi kwenye michezo miwili iliyosalia kwenye kundi lao.

Kapuru amesema wamepoteza mchezo huo kwa idadi kubwa ya mabao tangu mashindano hayo yaanze na sio jambo jema kwao.

Kwa upande wake kocha wa timu ya Nyasho,Omary Hamisi,amesema wachezaji wake wamefuata maelekezo yake na kupelekea kupata ushindi.

Mmoja wa waratibu wa mashindano hayo, Nyamuhanga Chome amesema tangu mashindano hayo yameanza yamekuwa na msisimko mkubws na yanaendelea vizuri.

Mapema saa 8 timu ya Nyamatare imechomoza na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Kwangwa ambapo kesho mashindano hayo ya Mathayo Cup yataendelea tena kwenye uwanja wa shule ya sekondari Musoma ambapo kwenye mchezo wa mapema saa 8 mchana timu ya Nyakato na Mshikamano zitskutana huku Rwamlimi na Bweri zikiumana saa 10 jioni.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!