Home Kitaifa KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI YARIDHISHWA NA MRADI...

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI YARIDHISHWA NA MRADI WA TIMIZA MALENGO.

Na Mwandishi Wetu – Morogoro

Kamati ya Kudumu ya Bunge inayosimamia Masuala ya UKIMWI, Kifua Kikuu , Dawa za Kulevya na Magonjwa yasiyoambukiza imeridhishwa na utekelezaji wa mradi wa Timiza Malengo unaotekelezwa na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) unaolenga kuwawezesha vijana kiuchumi.

Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya  UKIMWI, Kifua Kikuu , Dawa za Kulevya na Magonjwa yasiyoambukiza ikimsikiliza mnufaika wa mradi wa Timiza Malengo  ambaye anafanya biashara ya kuuza baiskeli (hazipo pichani) Bi. Nuru Nyatuka  wakati wa ziara hiyo.

Hayo yalisemwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dkt. Alice Kaijage wakati wa ziara ya Kamati ilipotembelea na kukagua utekelezaji wa mradi huo katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro ambapo alisema kuanzishwa kwa mradi kumewafanya vijana kuamka kifikra na kuamini wana uwezo wa kujieletea maendeleo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya  UKIMWI, Kifua Kikuu , Dawa za Kulevya na Magonjwa yasiyoambukiza Dkt. Alice Kaijage  akifafanua jambo .

Mradi huo unatekelezwa ikiwa ni Awamu ya Pili kuanzia mwaka 2021 hadi mwaka 2023 katika Halmashauri za Wilaya 18 zilizopo katika Mikoa mitano ya Dodoma, Geita, Morogoro, Singida na Tanga ukihusisha vijana wanaotoka katika kaya masikini.

“Katika Halmashauri ya Ifakara tumekuta serikali na watendaji wanafanya kazi kwa bidii sana tumewaona vijana wana ujasiri, wamefungua miradi, biashara, wengine wanafuga kuku, nguruwe na kufungua magenge ni kwa sababu serikali kupitia watendaji imewawezesha vijana hawa na imewasaidia kuepuka vishawishi mbalimbali,” Alisema Dkt. Alice.

Baadhi ya wakazi wa Halimashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro wakifuatilia mkutano wa Kamati  hiyo uliofanyika katika Shule ya Msingi ya Mtoni.

Pia aliwataka vijana hao kusimamia malengo yao kwa kutumia vyema fedha walizopewa ili kuanisha miradi hatua itakayosaidia kuepuka vishawishi vitakavyosababisha kupata maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutokan an ahali duni ya Maisha.

“Afua mojawapo katika kutekeleza na kupambana na masuala ya UKIMWI ni afua ya ulielimishaji rika ambayo inahusika kukinga na kuelimisha wasichana rika balehe ili wajiamini na kupambana na maisha yao wenyewe pamoja na kuepuka vishawishi,”Alieleza Makamu Mwenyekiti huyo.

Naye Naibu Katibu Mkuu , Ofisi ya Waziri Mkuu , Sera, Bunge na Uratibu Bwa. Kaspar Mmuya alisema afua za UKIMWI hazitekelezwi na wizara moja pekee bali zinatekelezwa na wizara zote za kisekta na wadau wa ndani na nje ya Nchi .

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bwa. Kaspar Mmuya akizungumza wakati wa ziara ya Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya  UKIMWI, Kifua Kikuu , Dawa za Kulevya na Magonjwa yasiyoambukiza ilipotembelea na kukagua utekelezaji wa  mradi wa Timiza Malengo  katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro.

“Malengo ya Serikali katika kupambana na UKIMWI imejielekeza ifikapo mwaka 2030 kusiwe na maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI na pasiwepo na mtu yeyote mwenye virusi vya UKIMWI ambaye atakufa kwa ugonjwa huo pamoja na kuondoa unyanyapaa ifikapo mwaka 2030,”Alibainisha Bwa. Mmuya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dkt. Leonard Maboko alifafanua tume hiyo inashirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambapo ina mtaala wa uelimishaji rika ambao unafundishwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari katika Halmashauri 18.

Mnufaika wa mradi wa Timiza Malengo Bi. Ebina Hassan Issa akitoa maelezo kwa kamati hiyo ilipomtembelea kujionea utekelezaji wa shughuli zake.

Vilevile Mkuu wa Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro Bi. Hanji Godigodi aliipongeza Serikali kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za taasisi za serikali na binafsi zinazopambana kudhibiti maambukizi ya virusi vya UKIMWI huku akiwataka watendaji kusimamia fedha za mradi ili kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.

Aidha Mmoja wa wanufaika wa mradi huo Bi. Gladness Champunga aliishukuru serikali na TACAIDS kwa kuanzisha mradi akisema umemnufaisha kama kijana kujipatia kipato kupitia saluni yake ambapo inamuwezesha kukidhi mahitaji muhimu.

MWISHO

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!