Home Afya KAGERA KUENDELEA NA MAPAMBANO  KUPUNGUZA MAAMBUKIZI DHIDI  YA  MALARIA.

KAGERA KUENDELEA NA MAPAMBANO  KUPUNGUZA MAAMBUKIZI DHIDI  YA  MALARIA.

Theophilida Felician Kagera.

Mkoa Kagera ukiwa ni miongoni mwa mikoa yenye kukabiliwa na changamoto ya maambukizi ya  ugonjwa tishio wa malaria mratibu wa malaria Mkoa Dkt Carlos  Christian Jackison amesema jitihada mbalimbali zinaendelea ili kuweza kuudhibiti ugonjwa huo ipasavyo.

Akizungumza na Mzawa Online katika Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa Bukoba iliyopo Manispaa ya Bukoba  amesema Kagera ni  Mkoa wa tatu  kuongoza kwa  maambukizi ya malaria nchini ambapo mwaka 2023 Halmashauri ya Ngara iliyoongoza kwa kiwango kikubwa cha maambukizi ambayo ilikuwa na asilimia 49%, ikafuatia Bukoba DC asilimia  41% .

Aidha Dkt Carlos amesema Halmashauri Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba imejitahidi kuwa na asilimia ndogo ya maambukizi ya ugonjwa huo na kwa mwaka huu kwa takwimu za Januari na aprili zinaonesha maambukizi yanaendelea kupungua kidogo japo Ngara inaendelea kuongoza kati Halmashauri zenye maambukizi.

Dkt Carlos  amesema sababu walizozibaini zinazoendelea kuchochea maambukizi  ni pamoja na matumizi  yasiyo sahihi ya vyandarua vyenye dawa , wagonjwa  kuchelewa kufika vituo vya kutolea huduma za tiba, mvua nyingi inayonyesha kwa misimu miwili kwa muda mrefu nakupelekea maji kutuwama  maeneo mengi  nakusababisha kuzaliana kwa mbu wa ambukizao malaria aina ya Anopheles.

Aidha Dkt Carlos amesema wanaendelea kuhamashisha jamii kuzingatia hatua mbalimbali  kutoka kwa watalaamu wa afya hususani  matumizi ya vyandarua, kuteketeza mazalia ya mbu kwakufukia mashimo yanyekutuwama maji, kufyeka nyasi, kuchoma chupa, kufika mapema Hopispitalini wanapohisi kuumwa, kutoa elimu kwa wajawazito ili kuwahi na kuhudhuria Kliniki kupewa  dawa za “SP”matumizi sahihi ya dawa ikiwa ni sambamba na kufanya vipimo kabla ya kutumia dawa.

Dkt Carlos amesema Malaria ipo ya aina mbili ipo  kali na isiyo kali, malaria kali  dalili zake  ni kuumwa kichwa, viongo vya mwili kuuma, kukosa hamu ya kula, tumbo kuuma, kuharisha na kutapika.

Malaria kali  dalili zake ni degedege, kutapika kila kitu, mwili kuishiwa nguvu kusiko kawaida na kuchanganyikiwa pia ni ugonjwa ambao umekuwa ukiwaathiri pakubwa  watoto na wajawazito.

Vilevile Dkt Carlos amewashukuru wadau wote wanaounga juhudi za kupambana na ugonjwa huo kwa Mkoa wa Kagera.

Hata hivyo Dkt Carlos amesema lengo la serikali ni kuhakikisha malaria inabakia “0” ifikapo 2030 kwani inawezekana iwapo kila mmoja atawajibika kuutokomeza.

Aidha Dkt Carlos Ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuzingatia maelekezo wanayopewa na watalaamu wa afya  badala yakuyapuuza kwani  malaria ni miongoni mwa magonjwa hatarishi  huku akiwahimiza  watalaamu  wa afya ngazi ya jamii kuendelea kuwafikia wananchi na kuwapa elimu kama ilivyokusudiwa na serikali.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!