Home Kitaifa JENERALI MABEYO AWAVISHA VYEO MAKAMISHNA WAPYA NCAA

JENERALI MABEYO AWAVISHA VYEO MAKAMISHNA WAPYA NCAA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) Jenerali Venance Mabeyo (Mstaafu) tarehe 29 Aprili, 2024 amewavisha vyeo maafisa Uhifadhi wakuu waliopandishwa vyeo hivi karibuni katika tukio lililofanyika ofisi za Makao makuu ya NCAA Karatu Mkoani Arusha.

Waliovishwa vyeo ni Afisa Uhifadhi Mkuu Lilian Magoma ambae amepandishwa na kuvishwa cheo kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya Mipango, tathmini na ufuatiliajI na Afisa Uhifadhi Mwandamizi wa Rasilimali watu Salma Chisonga aliyepandishwa cheo amevishwa cheo kuwa Kamishna msaidizi Mwandamizi wa uhifadhi, Rasilimali watu na Utawala.

Jenerali Mabeyo amewataka makamishna wapya kufanya kazi kwa kujituma na kuzingatia viapo vyao katika misingi ya uzalendo, maadili ya utumishi, ushirikiano, maarifa na bidii ya kazi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!