Home Kitaifa “DAMU CHAFU” IMEMALIZWA KATAVI.

“DAMU CHAFU” IMEMALIZWA KATAVI.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani amekiambia Chama Cha Mapinduzi kuwa ndani ya miezi minne wamefanikiwa kutokomeza kundi la uporaji na uhalifu maarufu kama “damu Chafu“.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mpanda mjini, Kamanda Ngonyani amemuambia Katibu wa NEC itikadi,uenezi na mafunzo Paul Makonda kuwa kundi hilo lilikuwa linahusisha watoto wa umri wa miaka 18-24.

Kamanda Ngonyani ametoa kauli hiyo baada ya Mwenezi Makonda kupata malalamiko kuhusu kundi hilo la wahalifu na kulingana na Jeshi la Polisi tayari vijana zaidi ya 60 walibainika na kuchukuliwa hatua.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!