Home Kitaifa BARUTI NI HATARI USIHIFADHI KWENYE JOTO, MOTO UMEME AU MOTO WA GASI

BARUTI NI HATARI USIHIFADHI KWENYE JOTO, MOTO UMEME AU MOTO WA GASI

Baruti haitakiwi kuhifadhiwa kwenye makazi ya watu kwasababu inaweza kulipuka kwa moto, joto, tayari moto wa gesi au umeme.

Hayo yamesemwa na Mhandisi Mgodi wa Geita Gold Mines GGM Katambala Abeli wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika Banda la Chamber of mines huko Dodoma kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Madini mwaka 2024 katika viwanja vya ukumbi wa Jakaya Kikwete convention center.

Amesema kwasababu wapo kwenye wiki ya madini ambapo hukutanishwa na Wachimbaji wameona wazungumzie hatari iliyo katika baruti.

Baruti ni moja ya nyenzo kuu inayotumika kuvunjia miamba migodini, katika Mgodi hauwezi kuvunja miamba mpaka utumie baruti” alisema Katambala.

Baruti ina madhara makubwa isipohifadhiwa katika mazingira na hali stahiki kama sheria za nchi zinavyoonyesha kwani haitakiwi kuwekwa pamoja na makazi ya watu kwani inaweza kuripuka

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!