Home Kitaifa ACT WAZALENDO YAUNDA KAMATI YA ILANI YA UCHAGUZI 2025, EMMANUEL MVULA KUONGOZA

ACT WAZALENDO YAUNDA KAMATI YA ILANI YA UCHAGUZI 2025, EMMANUEL MVULA KUONGOZA

Kiongozi wa Chama Cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu, ameunda Kamati ya Kuunda Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2025, ambapo amefanya uteuzi wa wajumbe 12 pamoja na sekretarieti 4.

Katika taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Kiongozi wa Chama hicho, tarehe 6 Februari 2025, jijini Dar es Salaam, Emmanuel Lazarus Mvula ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, huku Idrisa Kweweta akiteuliwa kuwa Katibu wa Kamati.

Emmanuel Mvula:
Mvula amewahi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Sera na Utafiti Taifa (2016-2019), Mjumbe wa Kamati Kuu ya ACT Wazalendo (2019-2024), na pia Mjumbe wa Kamati ya Maadili Taifa (2024 – hadi sasa). Aidha, amewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Timu ya Ushindi Taifa (2020) katika Kampeni za Chama. Mvula pia alikua Mjumbe wa Kamati ya Kuandaa Ilani ya Uchaguzi ya 2015-2020 na Mjumbe wa Kamati Kuu 2020-2024.

Idrisa Kweweta:
Kweweta amewahi kuwa Katibu wa Kamati ya Sera na Utafiti Taifa (2016-2019) na pia Katibu wa Sera, Utafiti na Mafunzo Taifa (2019-2024). Amefanya kazi kama Meneja wa Mafunzo katika Timu ya Ushindi ya Taifa (2020) na Mratibu wa Tafiti za Uchaguzi (2016-2024). Alikuwa Mkuu wa Sera na Utafiti katika Baraza Kivuli la Mawaziri (2022-2023), na Katibu Mkuu Kiongozi wa Baraza Kivuli la Mawaziri la ACT Wazalendo (2023).

Dkt. Elizabeth Sanga

Abdul Nondo

Prof. Omar Fakih

Yasinta Cornell Awiti

Mary Mongi

Seif Suleiman Hamad

Mtutura Abdallah Mtutura

Shangwe Ayo

Pavu Abdallah

Humphrey Mrema

Edgar Mkosamali

Maharagande Mbarala

Mshenga Juma

Jackline Prosper Ndonde

Jasper Sabuni

Said Mahalifa

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!