Home Kitaifa CHATANDA AKEMEA TABIA ZINAZOKWAMISHA WATOTO KUSHINDWA KUENDELEA NA MASOMO

CHATANDA AKEMEA TABIA ZINAZOKWAMISHA WATOTO KUSHINDWA KUENDELEA NA MASOMO

📍28 DISEMBA, 2024 – IRINGA

Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg Mary Pius Chatanda (MCC) amewataka wazazi kuacha mara moja tabia ya kuozesha watoto wakiwa na umri mdogo au kuwasafirisha mikoani kwenda kufanya kazi za ndani.

Akizungumza na wananchi wa Igowole mkoa Iringa, Chatanda amesema;

“Rais Samia ametengeneza na kuboresha miundombinu mizuri ya shule, ameajiri walimu wa kutosha na kuongeza vifaa ikiwemo vitabu kwasababu anataka watoto wasome katika mazingira mazuri ili waweze kufaulu, waweze kuajirika na kuajiriwa na waweze kujitegemea kiuchumi. Mkiwaozesha watoto wadogo au kuwapeleka kufanya kazi za ndani, mnakosea sana”

Chatanda amepiga marufuku tabia hii kwani inawanyima watoto haki ya kupata elimu na inakwamisha jitihada za kuwainua kiuchumi Watanzania wote ususani watoto wakike zinazofanywa na Serikali ya CCM kupitia Ilani yake ya Uchaguzi 2020/2025.

uwt imara

wanawake jeshi kubwa

kaziiendelee

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!