Afisa Habari wa wakala wa usajili Biashara na Leseni (BRELA) Gloria Mbilimonyo amesema kutokana na ukuaji wa Viwanda katika Jiji la Mwanza kupitia Maonesho ya 18 ya Biashara ya Afrika Mashariki NIC Mwaka huu yana kauli Mbiu isemayo Mazingira Bora ya Biashara ni kitovu Cha Kukuza Uwekezaji wa Biashara, Viwanda na Kilimo Afrika Mashariki kupitia Maonesho haya BRELA wamejipanga kutoa huduma za papo kwa hapo ya usajili wa Biashara Leseni, Viwanda na alama za Biashara.
Aliongeza kusema kuwa pia wanaendelea kuboresha huduma zao ziwe rafiki na gharama nafuu Kwa kuwepo na Usajili wa Makampuni kwa njia ya Mtandao.