Home Kitaifa WAZIRI WA MAMBO YA NJE INDIA AFANYA ZIARA DIT , AWAPONGEZA KWA...

WAZIRI WA MAMBO YA NJE INDIA AFANYA ZIARA DIT , AWAPONGEZA KWA TEKNOLOJIA ( + VIDEO )

WAWEZA KUTAZAMA VIDEO PIA

Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) imepongezwa kwa kuwa miongoni mwa Taasisi za Elimu Tanzania yenye ushirikiano mwema na nchi ya India kwenye masuala ya Teknolojia ya habari na mawasiliano.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya nje wa India Dkt.Sabrahmanyam Jaishankar katika ziara yake DIT alipotembelea kituo cha Umahiri cha Tehama (ITCoEICT) kwa ajili ya kuona maendeleo ya Tehama yaliyofikiwa.

Katika ziara yake Mhe Waziri amefurahishwa kusikia mafanikio yaliyofanyika kwenye kituo ikiwemo kutoa elimu pamoja na huduma za Tehama kwenye sekta binafsi, Elimu,kilimo na afya pamoja na mamlaka za hali ya hewa.

“Nimefahamishwa kusikia supercomputer ambayo ni Teknolojia ya haraka kuwa  zinatumika na  zimeweza kusaidia baadhi ya watafiti toka Chuo kikuu cha Dar es Salaam pamoja na Taasisi nyingine nyingi  za elimu haya ni mafanikio makubwa kwa DIT na kwetu hivyo ninafurahi na kupongeza juhudi hizi nina uhakika juhudi hizi zinazofanyika zitasaidia kufika mbali hasa kwenye Teknolojia.amesema Dkt.Jaishankar

Dkt.Jaishankar amesema amelisikia ombi la DIT kuhusu kuboresha na kuinua zaidi supercomputer na kuahidi kulifanyia kazi kwa kuwa maendeleo ya  kituo yanaridhisha na hana shaka

“Nimepewa taarifa kuhusiana na ombi lenu la kuboresha supercomputer niseme kuwa nimelipokea kwa furaha na niahidi kuwa ombi hili litafanyiwa kazi”amesema Dkt. Jaishankar

Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof.Adolf Mkenda amesema kuwa, Wanafunzi wanaohitimu elimu ya Sekondari na kufanya vizuri katika masomo ya Sayansi mwaka huu watapata ufadhili kwenda kusoma katika Chuo Kikuu cha Teknolojia cha India (IIT) kinachotarajia kuanzishwa tawi lake Zanzibar, kupitia Mfuko wa ufadhili wa Elimu wa Samia.

Waziri amesisitiza kuwa, atahaikikisha kwamba wanatoa mikopo na ufadhili wa masomo kupitia Mfuko wa Samia ili wanafunzi wakasome Zanzibar katika fani hiyo ambayo ni muhimu kwa Taifa.

“Kuanzia Oktoba au Novemba mwaka huu tunaanza kuchukua wanafunzi  50 wa shahada ya kwanza na 25 wa Shahada ya Uzamili wale wanafunzi waliomaliza kidato cha sita mwaka huu na kufanya vizuri sana wanaweza kuomba kusoma shahada katika chuo hiki.”amesema Prof.Mkenda 

Nae Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Mhandisi Dk Richard Masika amefurahishwa na ujio wa Waziri wa Mambo ya nje wa India  Subrahmanyam Jaishankar alipowasili katika taasisi hiyo na kukagua kituo cha Umahiri cha Tehama  (ITCoEICT) kilichoanzishwa mwaka 2009.

Amesema kituo hiki kimekuwa ni lango la teknolojia kwa kutoa huduma za tehama inayokuwa  kwa kasi zaidi nchini.

Amesema ushirikiano  na India ni kwa ajili ya kuboresha teknolojia  ziweze kuendana na maendeleo ya tehama nchini ikiwepo katika huduma za kilimo, jeshi na utabibu kwa njia ya mtandao kwa kutumia tehama.

Dk Masika amesema hiyo itakwenda kusaidia vijana wenye mawazo mbalimbali madogo kuwawezesha kuwapa elimu ya msingi katika kuwalengesha kwenye maeneo waliojikita. 

“Kwa sasa hivi kuna teknolojia mpya zimeingia ikiwepo mapinduzi ya viwanda kutoka taaluma hadi zana za kazi hivyo ujio wa taasisi ya teknolojia ya India itasaidia kupandisha ubora wa Teknolojia kwa vijana wa kitanzania wanaopita DIT kupata kwa ajili ya mafunzo”.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!