Home Kitaifa SERIKALI IPO KATIKA HATUA ZA MWISHO ZA KUKAMILISHA SERA YA TEHAMA

SERIKALI IPO KATIKA HATUA ZA MWISHO ZA KUKAMILISHA SERA YA TEHAMA

Naibu katibu mkuu wa wizara ya habari mawasiliano na tekmolojia ya Habari selestine Kakele amesema serikali ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha mapitio ya maboresho ya sera ya Tehama ili kuweza kuwezesha biashara za kimataifa kufanyika kidijiti

Ameyasema hayo katika maonesho ya sabasaba baada ya kutembelea banda la shirika la mawasiliano nchini TTCL ambapo amebainisha kuwa shirika hilo limepiga hatua katika utoaji na usambazaji wa huduma za mawasiliano ya internet nchini

“kukamilika kwa sera yetu kunazidi kujenga mazingira mazuri ya kuvutia uwekezaji hapa nchini, si tu katika tehama lakini katika sekta nyingine za kijamii na kiuchumi tukizungumzia afya, kilimo na elimu”

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here
Captcha verification failed!
CAPTCHA user score failed. Please contact us!